I WILL BE BACK 7
Ilikua ni siri kubwa sana halafu nzito, siri iliyotutoa machozi mimi pamoja na yule Joel kijana wa kizungu ambaye alikua amemdanganya mpenzi wake kuwa walikua wakienda nchini Tanzania kutalii kumbe nyuma ya pazia Joel alikua na kazi kubwa sana ya kuifanya kwa ajili ya kutimiza maagizo aliyokua ameachiwa na marehemu mama yake.
Lakini licha ya siri ile kututoa machozi lakini ilionekana kufanana baadhi ya matukio kiasi cha kufanya na mimi nione kuwa nilikuwa nikihusika katika ile mission ya Joel kwa ajili ya kuyaekeleza maagizo aliyokua ameachiwa na marehemu mama yake.
Joel Poesmark hakua akija nchini Tanzania kwa lengo la kutalii kama alivyo mdanganya mpenzi wake ambaye muda wote ule alikua hajielewi kwa sababu ya kupitiwa na uisngizi mzito uliozichukua fahamu zake kama ilivyokua kwa abiria wengine.
Joel alikua anakuja nchini Tanzania kwa ajili ya kulipiza kisasi kwa kijana wa kikongo aliyekimbilia nchini Tanzania kutokea katika nchi ya Kongo mara baada ya kumuua baba yake Mr.Poesmark aliyetoka nchiniUingereza miaka miwili iliyopita na kwenda nchini Kongo ambapo alifungua biashara kubwa ya kuuza magari yaliyotumika kutoka nchini Japani na kuyasambaza katika nchi za Kongo pamoja na Angola.
Biashara ile ilionekana kumlipa sana Mr.poesmark na kumpatia utajiri mwingi sana uliomtoa udenda kijana yule wa kikongo ambaye aliamua kumuua Mr.poesmark na kuiba mali zake zote karibu dola million 2 za kimarekani ambazo ni sawa na shilingi bilioni tatu na milioni mia 2 za Tanzania.
Kitendo cha Joel kuniambia kuwa alikua anakuja nchini Tanzania kumtafuta yule raia wa Kongo aliyekua amemuua baba yake na kuiba mali zake kilinishtua sana na kufanya niyakumbuke yale maneno ya bwana James kaka yake na yule mzungu mdogo Slyvester niliekua nikisafiri nae ndani ya ndege moja ambapo yeye alikua anakwenda nchini Kenya.
“All of you’re companies are selled to a guy from Congo who called Motemapembe”
(makampuni yako yote yameuzwa kwa mtu mmoja kutoka Kongo aitwaye Motemapembe)
Yalikua ni maneno ya rafiki yangu kipenzi James siku nilipoongea nae baada ya kukutana nae pale Nanning airport usiku muda mfupi kabla sijaianza safari yangu ya kurejea nyumbani.
Akili zangu zilishtuka sana licha ya kutomwambia Joel lakini akilini kwangu ilianza kunijia picha kuwa huenda yale makampuni yangu yote mawili ya usafirishaji alikua ameyanunua huyo mkongo kutoka kwa mke wanguTressy aliyeamua kuyaharibu maisha yangu kwa kuniacha bila sababu na kuamua kuyatia umaskini maisha yangu kwa kuziuza mali zangu zote nilizokua nikizitegemea sana katika kuniingizia kipato.
“I think I know this bastard who you talking about”
(nadhani ninamfahamu uyu mwanaharamu unaemuongelea)
Nilimwambia Joel na kumfanya aghutuke sana , nilimwambia huku nikifuta machozi yaliyonitoka hasa baada ya akili zangu kuanza kuamini kuwa huenda ikawa huyo mkongo aliyenunua makampuni yangu yote mawili ya usafirishaji kutoka kwa Tressy.
“Are you sure?”
(Una uhakika) Joel aliniambia mara tu baada ya mimi kumwambia kuwa huenda ninamfahamu huyo mwanaharamu aliyekua akimuongelea.
“Im not sure yet but as I told you, my wife betrayed and sells all of my companies and according to Mr James told me all this, that the buyer of my companies is a guy from Congo”
(sina uhakika sana lakini kama nilivyokwambia mke wangu amenisaliti kwa kuyauza makampuni yangu yote na kwa mujibu wa Mr James aliyeniambia haya yote mnunuzi wa makampuni yangu ni mtu kutoka Kongo)
Nilimwambia Joel ambaye alikua ametulia huku akinisikiliza kwa makini sana
“Is it possible?"
(inawezekana?) Joel aliniuliza baada ya mimi kumaliza kuongea kabla hata sijameza fundo la mate.
“Yeah it possible because as you told me that your father was the cars seller and supplier and my companies were dealings with transportation don’t you think there is something match here”
(Yeah inaweza kuja kama ulivyoniambia kuwa baba yako alikua muuzaji na msambazaji wa magari halafu mimi nilikua namiliki kampuni za usafirishaji huoni kama kunakitu kinataka kufanana)
“May be your right but I remember let me show you the picture of that guy which my mother gave to me before he die”
(unaweza kuwa sahihi lakini nimekumbuka ngoja nikuonyeshe picha ya huyo mtu ambayo mama yangu aliniachia kabla hajafariki)
Joel aliniambia huku akikagua mifuko ya koti lake zito alilokua amelivaa kutokana na baridi iliyosababishwa na hali ya hewa ya pale jijini Beijing.
Ilikua ni saa 11 karibu na nusu, Joel alikua bize kuikagua mifuko ya koti lake, kuitafuta picha ya huyo mkongo aliyesadikika kumuua baba yake kutokana na maelezo ya marehemu mama yake na Joel.
Ghafla!! Akiwa katika kuikagua mifuko yake sauti ya kike ilisikika kutoka upande wa pili wa viti tulipokua tumekaa.
“Baby you are not sleep?”
(mpenzi haujalala) ilikua ni sauti ya mpenzi wake na Joel aliyeuamka usingizini muda mchache uliopita.
Kitendo cha mpenzi wa Joel kuamka kiliashiria kuwa huo ndio ulikua mwisho wa maongezi yangu na Joel na baada ya yeye kuamka mimi nilijidai kukoroma kana kwamba nilikua katika usingizi mzito sana nilifanya hivi ili kumzuga kua hakuna kitu chochote kilichokua kinaendelea kati yangu na Joel
ZzZzZz ZzZzZ!! KROWH KROWH nilikoroma kana kwamba nilikua usingizini kumbe nilikua nikimzuga huyo mpenzi wake na Joel aliyetoka kushtuka kutoka usingizini muda mfupi uliopita.
“Baby plz just try to sleep even one hour otherwise youn will tired”
(mpenzi basi jaribu kulala hata saa moja lasivyo utachoka sana)
Sauti laini ya huyo mpenzi wa Joel ilimsihi Joel ajaribu kulala kwa baada ya kufumwa na mpenzi wake akiwaa macho anatafuta picha ya yule mwanaharamu kutoka Kongo kwa ajili ya kunionyesha.
Nilikua mzugaji mzuri, niliongeza tena sauti yangu ya kukoroma kwa makusudi ili kuharibu maongezi yao mara baada ya kumpiga Joel kajicho upande na kumuona kua alikua ameshaanza kuchoka na maongezi ya mpenzi wake ambaye sikua nikimfahamu jina lake
Nilifanya hivi kwa lengo la kupata tena nafasi ya kuongea na Joel, nilikua na hamu kubwa sana ya kumuona huyo mkongo ambaye tulikua tukimuongelea, lakini pia niliingiwa na wivu, mapenzi yao yalinikumbusha Tressy wangu ambae alikua amenipiga changa la macho, kunisaliti na kuuza mali zangu zote.
“why this guy sound like the frog”
(kwanini huyu anakoroma kama chura)
Yule mpenzi mtoto wa kike alimuuliza mpenziwe Joel, kelele zangu zilimkera.
"may be he tired"
(labda amechoka)
Joel alimwambia mpenzi wake huku akijua wazi kua tulikua tukimchezea huyo mtoto wa kike picha la kihindi.
Na wakati hayo yote yanaendelea mimi nilikua nikitabasamu kimoyomoyo kwani mission yangu ndogo ya kumuokoa Joel ilikua imeshafanikiwa na kuwafanya bwana Joel na mpenzi wake waache mazungumzo yao.
Je nini kitatokea ……………………?
Usikose sehemu zinazoendelea
ITAENDELEA……………….
Ilikua ni siri kubwa sana halafu nzito, siri iliyotutoa machozi mimi pamoja na yule Joel kijana wa kizungu ambaye alikua amemdanganya mpenzi wake kuwa walikua wakienda nchini Tanzania kutalii kumbe nyuma ya pazia Joel alikua na kazi kubwa sana ya kuifanya kwa ajili ya kutimiza maagizo aliyokua ameachiwa na marehemu mama yake.
Lakini licha ya siri ile kututoa machozi lakini ilionekana kufanana baadhi ya matukio kiasi cha kufanya na mimi nione kuwa nilikuwa nikihusika katika ile mission ya Joel kwa ajili ya kuyaekeleza maagizo aliyokua ameachiwa na marehemu mama yake.
Joel Poesmark hakua akija nchini Tanzania kwa lengo la kutalii kama alivyo mdanganya mpenzi wake ambaye muda wote ule alikua hajielewi kwa sababu ya kupitiwa na uisngizi mzito uliozichukua fahamu zake kama ilivyokua kwa abiria wengine.
Joel alikua anakuja nchini Tanzania kwa ajili ya kulipiza kisasi kwa kijana wa kikongo aliyekimbilia nchini Tanzania kutokea katika nchi ya Kongo mara baada ya kumuua baba yake Mr.Poesmark aliyetoka nchiniUingereza miaka miwili iliyopita na kwenda nchini Kongo ambapo alifungua biashara kubwa ya kuuza magari yaliyotumika kutoka nchini Japani na kuyasambaza katika nchi za Kongo pamoja na Angola.
Biashara ile ilionekana kumlipa sana Mr.poesmark na kumpatia utajiri mwingi sana uliomtoa udenda kijana yule wa kikongo ambaye aliamua kumuua Mr.poesmark na kuiba mali zake zote karibu dola million 2 za kimarekani ambazo ni sawa na shilingi bilioni tatu na milioni mia 2 za Tanzania.
Kitendo cha Joel kuniambia kuwa alikua anakuja nchini Tanzania kumtafuta yule raia wa Kongo aliyekua amemuua baba yake na kuiba mali zake kilinishtua sana na kufanya niyakumbuke yale maneno ya bwana James kaka yake na yule mzungu mdogo Slyvester niliekua nikisafiri nae ndani ya ndege moja ambapo yeye alikua anakwenda nchini Kenya.
“All of you’re companies are selled to a guy from Congo who called Motemapembe”
(makampuni yako yote yameuzwa kwa mtu mmoja kutoka Kongo aitwaye Motemapembe)
Yalikua ni maneno ya rafiki yangu kipenzi James siku nilipoongea nae baada ya kukutana nae pale Nanning airport usiku muda mfupi kabla sijaianza safari yangu ya kurejea nyumbani.
Akili zangu zilishtuka sana licha ya kutomwambia Joel lakini akilini kwangu ilianza kunijia picha kuwa huenda yale makampuni yangu yote mawili ya usafirishaji alikua ameyanunua huyo mkongo kutoka kwa mke wanguTressy aliyeamua kuyaharibu maisha yangu kwa kuniacha bila sababu na kuamua kuyatia umaskini maisha yangu kwa kuziuza mali zangu zote nilizokua nikizitegemea sana katika kuniingizia kipato.
“I think I know this bastard who you talking about”
(nadhani ninamfahamu uyu mwanaharamu unaemuongelea)
Nilimwambia Joel na kumfanya aghutuke sana , nilimwambia huku nikifuta machozi yaliyonitoka hasa baada ya akili zangu kuanza kuamini kuwa huenda ikawa huyo mkongo aliyenunua makampuni yangu yote mawili ya usafirishaji kutoka kwa Tressy.
“Are you sure?”
(Una uhakika) Joel aliniambia mara tu baada ya mimi kumwambia kuwa huenda ninamfahamu huyo mwanaharamu aliyekua akimuongelea.
“Im not sure yet but as I told you, my wife betrayed and sells all of my companies and according to Mr James told me all this, that the buyer of my companies is a guy from Congo”
(sina uhakika sana lakini kama nilivyokwambia mke wangu amenisaliti kwa kuyauza makampuni yangu yote na kwa mujibu wa Mr James aliyeniambia haya yote mnunuzi wa makampuni yangu ni mtu kutoka Kongo)
Nilimwambia Joel ambaye alikua ametulia huku akinisikiliza kwa makini sana
“Is it possible?"
(inawezekana?) Joel aliniuliza baada ya mimi kumaliza kuongea kabla hata sijameza fundo la mate.
“Yeah it possible because as you told me that your father was the cars seller and supplier and my companies were dealings with transportation don’t you think there is something match here”
(Yeah inaweza kuja kama ulivyoniambia kuwa baba yako alikua muuzaji na msambazaji wa magari halafu mimi nilikua namiliki kampuni za usafirishaji huoni kama kunakitu kinataka kufanana)
“May be your right but I remember let me show you the picture of that guy which my mother gave to me before he die”
(unaweza kuwa sahihi lakini nimekumbuka ngoja nikuonyeshe picha ya huyo mtu ambayo mama yangu aliniachia kabla hajafariki)
Joel aliniambia huku akikagua mifuko ya koti lake zito alilokua amelivaa kutokana na baridi iliyosababishwa na hali ya hewa ya pale jijini Beijing.
Ilikua ni saa 11 karibu na nusu, Joel alikua bize kuikagua mifuko ya koti lake, kuitafuta picha ya huyo mkongo aliyesadikika kumuua baba yake kutokana na maelezo ya marehemu mama yake na Joel.
Ghafla!! Akiwa katika kuikagua mifuko yake sauti ya kike ilisikika kutoka upande wa pili wa viti tulipokua tumekaa.
“Baby you are not sleep?”
(mpenzi haujalala) ilikua ni sauti ya mpenzi wake na Joel aliyeuamka usingizini muda mchache uliopita.
Kitendo cha mpenzi wa Joel kuamka kiliashiria kuwa huo ndio ulikua mwisho wa maongezi yangu na Joel na baada ya yeye kuamka mimi nilijidai kukoroma kana kwamba nilikua katika usingizi mzito sana nilifanya hivi ili kumzuga kua hakuna kitu chochote kilichokua kinaendelea kati yangu na Joel
ZzZzZz ZzZzZ!! KROWH KROWH nilikoroma kana kwamba nilikua usingizini kumbe nilikua nikimzuga huyo mpenzi wake na Joel aliyetoka kushtuka kutoka usingizini muda mfupi uliopita.
“Baby plz just try to sleep even one hour otherwise youn will tired”
(mpenzi basi jaribu kulala hata saa moja lasivyo utachoka sana)
Sauti laini ya huyo mpenzi wa Joel ilimsihi Joel ajaribu kulala kwa baada ya kufumwa na mpenzi wake akiwaa macho anatafuta picha ya yule mwanaharamu kutoka Kongo kwa ajili ya kunionyesha.
Nilikua mzugaji mzuri, niliongeza tena sauti yangu ya kukoroma kwa makusudi ili kuharibu maongezi yao mara baada ya kumpiga Joel kajicho upande na kumuona kua alikua ameshaanza kuchoka na maongezi ya mpenzi wake ambaye sikua nikimfahamu jina lake
Nilifanya hivi kwa lengo la kupata tena nafasi ya kuongea na Joel, nilikua na hamu kubwa sana ya kumuona huyo mkongo ambaye tulikua tukimuongelea, lakini pia niliingiwa na wivu, mapenzi yao yalinikumbusha Tressy wangu ambae alikua amenipiga changa la macho, kunisaliti na kuuza mali zangu zote.
“why this guy sound like the frog”
(kwanini huyu anakoroma kama chura)
Yule mpenzi mtoto wa kike alimuuliza mpenziwe Joel, kelele zangu zilimkera.
"may be he tired"
(labda amechoka)
Joel alimwambia mpenzi wake huku akijua wazi kua tulikua tukimchezea huyo mtoto wa kike picha la kihindi.
Na wakati hayo yote yanaendelea mimi nilikua nikitabasamu kimoyomoyo kwani mission yangu ndogo ya kumuokoa Joel ilikua imeshafanikiwa na kuwafanya bwana Joel na mpenzi wake waache mazungumzo yao.
Je nini kitatokea ……………………?
Usikose sehemu zinazoendelea
ITAENDELEA……………….
COMMENTS